Makala Maalum
Msaada wa Kibinadamu
Mratibu Mkuu wa Misaada ya Dharura wa Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Wakimbizi wamezindua ombi la pamoja la msaada wa kibinadamu la jumla ya dola bilioni 6, tarehe 17 February 2025, ambalo ni ombi kubwa zaidi kuwahi kutolewa kwa ajili ya Sudan ili kusaidia takribani watu milioni 21ndani ya Sudan,pamoja na hadi watu milioni 5 wengine, wengi wao wakiwa wakimbizi waliokimbilia nchi jirani.
Habari kwa Picha
Kutoka jukwaani hadi doria za ulinzi mkali: Mapumziko baada ya wiki nyenye heka heka nyingi zaidi UN
Marais, Mawaziri Wakuu, Wakuu wananchi wanaelekea nyumbani baada ya kumalikiza kwa wiki ya mikutano ya ngazi ya juu katika Umoja wa Mataifa. Wiki hiyo ilisheheni kauli zilizotolewa na kila nchi wanachamakatika Mjadala Mkuu wa 80 pamoja na mikutano mingi muhimu kuhusu masuala muhimu duniani.
Habari Nyinginezo
Amani na Usalama
Nchini Sudan Kusini, matumaini mapya yamechipua baada ya watoto waliokuwa wametumikishwa kwenye jeshi la nchi hiyo, SSPDF kuachiliwa rasmi katika hafla iliyoungwa mkono na Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, UNMISS. Tukio hilo limeelezwa kuwa ishara muhimu ya kumaliza utumikishaji wa watoto katika jeshi na kuwapa nafasi ya kujenga maisha mapya.
Tabianchi na mazingira
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) nchini Tanzania limeelezea jinsi warsha mbili ilizoendesha katika mikoa ya Tanga na Mtwara kuhusu dhana ya uchumi rejeshi zimeanza kuzaa matunda kwani sekta hiyo ina fursa kubwa za kiuchumi, kiteknolojia, na kimazingira.